Mkurugenzi
wa mradi wa Evidence for Action Craig Ferla akizungumza na waandishi wa habari
Tanzania wanaobobea kuandika habari za afya ya uzazi2012.
NA, GORDON KALULUNGA.
INATIA moyo kusoma makala hii ambayo inatoa mchango wake katika kuhamasisha jamii ya watanzania kufahamu ukubwa wa changamoto zinazowakabili mama zetu na vichanga wakati wa ujauzito na kujifungua.
INATIA moyo kusoma makala hii ambayo inatoa mchango wake katika kuhamasisha jamii ya watanzania kufahamu ukubwa wa changamoto zinazowakabili mama zetu na vichanga wakati wa ujauzito na kujifungua.
Katika tukio
hilo adhimu la kuleta uhai duniani inasikitisha mno kwamba akina mama na watoto
wachanga wengi hufariki hapa nchini.
Ni muhimu
pia kutolea ufafanuzi kuhusu baadhi ya taarifa zilizomo kwenye makala hii.
Shirika la
Afya Duniani linakadiria kuwa wanawake 8,500 na watoto wachanga 50,000 hapa
Tanzania hufariki kila mwaka katika kipindi cha ujauzito na kujifungua. Ni
takwimu za kushtusha sana.
Ni muhimu
kufafanua zaidi kuwa mtoto mchanga ni mwenye umri wa tangu siku 0 hadi 28,
ikiwa ni pamoja na wanaozaliwa wameisha kufa.
Kuna idadi
nyingine kubwa zaidi ya watoto walio chini ya miaka mitano ambao hufariki kila
mwaka (kama ilivyojumuishwa kwa makosa kwenye makala hii, badala ya vichanga
peke yake).
Ila
izingatiwe kuwa vifo vya watoto katika siku 28 za kwanza za kuishi ni karibu
theluthi moja ya vifo vyote vya watoto chini ya miaka mitano hapa Tanzania.
Ukichukua
takwimu za wastani wa wanawake 8,500 na vichanga 50,000 wanaofariki wakati wa
ujauzito na kujifungua kila mwaka nchini Tanzania, hii ni sawa na akina mama 23
na vichanga 137 wanaofariki kila siku.
Hili ni
janga, hasa ukizingatia kuwa wengi wa akina mama na vichanga hawa wangeweza
kuokolewa kama wangepata huduma bora.
Hata hivyo
ni vigumu kuona na kuzingatia uhalisia wa kiwango na wingi wa vifo hivi katika
maisha ya kila siku, hasa pale takwimu kubwa kama hizo zinapotumiwa.
Hivyo basi
ndiyo sababu ukawekwa mfano huu kueleza ukubwa wa janga hili la kuwapoteza mama
zetu na vichanga kila siku.
Ukisafiri
ndani ya Tanzania kwa usafiri wa anga, kawaida ndege zinazotumika ni zile zenye
kubeba abiria wapatao 30 hivi.
Na ndipo
tulipoona muafaka kutumia mfano wa vifo vya akina mama 23 na vichanga 137 kila
siku, kuwa ni kama ndege tano za abiria zingeanguka kila siku, ambapo kati ya
hizo ndege tano, ndege moja ingebeba akinamama na nyingine nne zingebeba vitoto
vichanga.
Kuielezea
hali kwa namna hii ni kwa nia ya kufikisha ujumbe wa ukubwa wa janga hili
linalozikumba familia na taifa kwa ujumla kila siku.
Hebu fikiria
kama kungekuwepo kweli na ajali tano za ndege kila siku—kungekuwa na taharuki
kubwa sana na wanajamii wa ngazi zote kulikemea jambo hili kudai likomeshwe
mara moja, huku juhudi za kila aina zingefanywa lisitokee tena.
Ili
kuboresha hali ya uzazi salama kwa kiwango kikubwa, ni muhimu sana wanawake
wengi zaidi watafute nakupata huduma bora.
Iwapo kila
mama atajifungulia kwenye kituo cha tiba ambacho kinatoa huduma bora, akina
mama wengi na vichanga tunaowapoteza kwa sasa wataokolewa. Kwa sasa wanawake
wanaojifungulia katika vituo vya afya bado ni wachache:
kwa mujibu
wa utafiti wa Demografia na Afya Tanzania (TDHS) 2010 ni mwanamke mmoja tu
katika kila wawili ndiye anayejifungulia katika kituo cha afya.
Yaani kigezo
cha hatua hii muhimu ambayo ingeweza kuchukuliwa na kupunguza vifo vya mama na
vichanga kwa kiasi kikubwa kimekuwa hivyo hivyo katika kipindi cha miaka 25
bila mabadiliko.
Hii ni tangu
ulipofanyika utafiti wa TDHS wa kwanza 1990 ambapo ni nusu tu ya wanawake
walikuwa wakijifungulia kwenye vituo vya afya.
Na japo kwa
usahihi kabisa, makala hii imeeleza kuhusu ongezeko la idadi ya vizazi hai
katika vituo vya afya, ieleweke kuwa pia ongezeko kubwa la idadi ya watu hapa
Tanzania linamaanisha kuwa mfumo wa afya nao haujaweza kufanya mabadiliko ya
kuendana na kiwango cha ongezeko la wanawake wanaojifungulia vituo vya afya
kati ya mwaka 1986 na 2010.
Ujumbe mkuu
hapa ni kuwa idadi kubwa ya akina mama na watoto wachanga wa Tanzania ambao
maisha yao yanapotea wakati wa ujauzito na kujifungua kila mwaka yangeweza, na
kwa hakika yanatakiwa kuokolewa.
Kila mtu,
kwa nafasi yake katika jamii ni lazima atambue fursa zilizopo, zinazoweza
kugeuza mwelekeo wa janga hili linalotokea kila siku.
No comments:
Post a Comment