JE UNA WATOTO NJE YA NDOA ULIOPATA BAADA YA KUFUNGA NDOA?
(a) Ndio na mke anajua (b) Ndio na mke hajui (c) Ndio na mume hajui
(d) Ndio mume anajua (e) Tulitoa mimba (f) Sina.
TOA MAONI YAKO KWA KUBOFYA NENO COMMENT KISHA ANDIKA JAWABU NA HATA KAMA UNA SABABU PIA....
Saturday 31 May 2014
JK to health workers: You can stop maternal and child deaths
Calling it a major national silent emergency, President Kikwete said it is a unacceptable that as many as 455 women out of every 100,000 live births die during delivery in a country boasting a comprehensive health system.
The president was giving his remarks during the launch of the ‘Tanzania countdown and a promise renewed on reproductive, maternal, newborn and child deaths’ in Dar es Salaam yesterday.
President Kikwete said while a lot has been achieved during the implementation of the Millenium Development Goals (MGDS) there were still sad stories of women and children who die for reasons which could be avoided.
He said the medical personnel and stakeholders must fight for increased utilisation of family planning services while also increasing the percentage of skilled health providers in the health sector.
He stated that many of the births were being conducted by traditional birth attendants who cannot handle delivery complications.
“We do not underrate the work done by these traditional birth attendants but measures must be taken to upgrade the qualifications of those dealing with helping pregnant mothers to deliver,” he said.
He asked the health ministry to make sure that men ware also included in programmes aiming to reduce maternal deaths in the country.
The president asked the health ministry to introduce Maternal, Newborn and Child Health (MNCH) scorecards in all regions in the country which will show the regional performance in dealing with maternal and child health care problems.
He said the scorecards would allow effective supervision of the activities on reproductive health activities in respective regions by health officials.
The president said he himself will want to get the regional reports every four months “and not in six months as some officials suggested.”
“Matters concerning maternal and child health are very close to my heart. I will therefore want to have these scorecards every four month to know those regions which perform well and those which underperform.
He commended Singida Region for making sure that life saving items for women and children were readily available in the region.
Tanzania is one of the ten countries contributing to 61 percent and 66 percent of the global total of maternal and newborn deaths, respectively.
According to sources maternal mortality ratios are lowest in Dar es Salaam, Arusha and Kilimanjaro regions.
Mtwara, Tabora, Tanga, Lindi and Pwani have institutional maternal mortality ratios exceeding 200 per 100,000 live births.
Meanwhile President Kikwete has observed that some of the non-governmental organisations were diverting funds meant for maternal and child health affairs.
“We have organisations, although not many, who use funds meant to help maternal and child health activities for their own benefit,” he said.
“Instead of healing many mothers and children they help their own children,” he noted.
SOURCE:
THE GUARDIAN
TACAIDS; WANAOSAMEHE HAWAPATI MAAMBUKIZI YA VVU
Afisa utafiti wa tume ya kudhibiti Ukimwi nchini(TACAIDS) Dr. Avoldia Mlokozi.
Na, Gordon Kalulunga
TUME ya
Kudhibiti UKIMWI nchini (TACAIDS) imesema wanandoa na watu walio kwenye
mahusiano, wakiwa na tabia ya kusameheana wanapokoseana, wanaweza kupunguza
ongezeko la maambukizi ya VVU.
Hayo
yalisemwa na afisa utafiti wa tume hiyo Dr. Avoldia Mlokozi alipozungumza na
waandishi wa habari Jijini Mbeya katika mohojiano maalum.
‘’Ukitaka
kuishi kwa usalama ni kuwa na msamaha kwa mwenzako badala ya kuchepuka kwenye
ndoa kwa kisingizio cha kuudhiwa na mwenza wako’’ alisema Dr. Mlokozi.
Alisema
katika kanda ya nyanda za juu kusnini magharibi, kiwango cha maambukizi ya VVU,
mkoa wa Mbeya una asilimia 9, Rukwa 6.2 na Katavi ni 5.9 kiwanga ambacho ni
kikubwa kuliko wastani wa taifa wa asilimia 5.1.
Alitanabaisha
kuwa katika maambukizi hayo, wanawake ndiyo walioathirika zaidi kwa kuwa na
maambukizi ya wastani wa asilimia 9.2 na wanaume asilimika 6.5 kwa takwimu za
utafiti wa mwaka 2011-2012.
‘’Wanawake
wanaopata zaidi ugonjwa huo ni wale wenye umri wa miaka kati ya 20 mpaka 30
kwasababu hao ndiyo wanakuwa kwenye mahusiano, kuolewa na kujifungua’’ alisema
Dr. Mlokozi.
Aliongeza
kwa kusema kwamba, tayari kuna mikakati ya elimu kwa lika hiyo ili kuweza
kupunguza ushamiri wa maambukizi hayo ya VVU kwa wanawake.
Kuhusu mkoa
wa Mbeya, alisema mkoa huo umeendelea kuathirika zaidi na ugonjwa huo kutokana na mwingiliano wa
watu kimaendeleo ikiwemo suala zima la uchumi ambapo baadhi ya wafanyabiashara
na madereva wanaotumia barabara kuu ya kutoka Dar es Salaam na kwenda Zimbabwe,
Malawi, Zambia, Kongo na kwingineko kusini mwa Afrika, wanalala katika mkoa huo
na kujiingiza katika mahusiano na baadhi hawatumii Kondomu.
‘’Nchi hizo
zina maambukizi kuliko ya hapa nchini, hivyo pia ni moja ya sababu ya kuendelea
kushamiri ugonjwa huo mkoani Mbeya na baadhi ya wanaume hawajafanyiwa tohara
ambayo inasaidia kupunguza maambukizi kwa asilimia 60 na magonjwa ya zinaa’’
alisema Dr. Mlokozi.
VIFO VYA WAJAWAZITO TANZANIA, SAWA NA AJALI TANO ZA NDEGE ZA ABIRIA KILA SIKU
Mkurugenzi
wa mradi wa Evidence for Action Craig Ferla akizungumza na waandishi wa habari
Tanzania wanaobobea kuandika habari za afya ya uzazi2012.
NA, GORDON KALULUNGA.
INATIA moyo kusoma makala hii ambayo inatoa mchango wake katika kuhamasisha jamii ya watanzania kufahamu ukubwa wa changamoto zinazowakabili mama zetu na vichanga wakati wa ujauzito na kujifungua.
INATIA moyo kusoma makala hii ambayo inatoa mchango wake katika kuhamasisha jamii ya watanzania kufahamu ukubwa wa changamoto zinazowakabili mama zetu na vichanga wakati wa ujauzito na kujifungua.
Katika tukio
hilo adhimu la kuleta uhai duniani inasikitisha mno kwamba akina mama na watoto
wachanga wengi hufariki hapa nchini.
Ni muhimu
pia kutolea ufafanuzi kuhusu baadhi ya taarifa zilizomo kwenye makala hii.
Shirika la
Afya Duniani linakadiria kuwa wanawake 8,500 na watoto wachanga 50,000 hapa
Tanzania hufariki kila mwaka katika kipindi cha ujauzito na kujifungua. Ni
takwimu za kushtusha sana.
Ni muhimu
kufafanua zaidi kuwa mtoto mchanga ni mwenye umri wa tangu siku 0 hadi 28,
ikiwa ni pamoja na wanaozaliwa wameisha kufa.
Kuna idadi
nyingine kubwa zaidi ya watoto walio chini ya miaka mitano ambao hufariki kila
mwaka (kama ilivyojumuishwa kwa makosa kwenye makala hii, badala ya vichanga
peke yake).
Ila
izingatiwe kuwa vifo vya watoto katika siku 28 za kwanza za kuishi ni karibu
theluthi moja ya vifo vyote vya watoto chini ya miaka mitano hapa Tanzania.
Ukichukua
takwimu za wastani wa wanawake 8,500 na vichanga 50,000 wanaofariki wakati wa
ujauzito na kujifungua kila mwaka nchini Tanzania, hii ni sawa na akina mama 23
na vichanga 137 wanaofariki kila siku.
Hili ni
janga, hasa ukizingatia kuwa wengi wa akina mama na vichanga hawa wangeweza
kuokolewa kama wangepata huduma bora.
Hata hivyo
ni vigumu kuona na kuzingatia uhalisia wa kiwango na wingi wa vifo hivi katika
maisha ya kila siku, hasa pale takwimu kubwa kama hizo zinapotumiwa.
Hivyo basi
ndiyo sababu ukawekwa mfano huu kueleza ukubwa wa janga hili la kuwapoteza mama
zetu na vichanga kila siku.
Ukisafiri
ndani ya Tanzania kwa usafiri wa anga, kawaida ndege zinazotumika ni zile zenye
kubeba abiria wapatao 30 hivi.
Na ndipo
tulipoona muafaka kutumia mfano wa vifo vya akina mama 23 na vichanga 137 kila
siku, kuwa ni kama ndege tano za abiria zingeanguka kila siku, ambapo kati ya
hizo ndege tano, ndege moja ingebeba akinamama na nyingine nne zingebeba vitoto
vichanga.
Kuielezea
hali kwa namna hii ni kwa nia ya kufikisha ujumbe wa ukubwa wa janga hili
linalozikumba familia na taifa kwa ujumla kila siku.
Hebu fikiria
kama kungekuwepo kweli na ajali tano za ndege kila siku—kungekuwa na taharuki
kubwa sana na wanajamii wa ngazi zote kulikemea jambo hili kudai likomeshwe
mara moja, huku juhudi za kila aina zingefanywa lisitokee tena.
Ili
kuboresha hali ya uzazi salama kwa kiwango kikubwa, ni muhimu sana wanawake
wengi zaidi watafute nakupata huduma bora.
Iwapo kila
mama atajifungulia kwenye kituo cha tiba ambacho kinatoa huduma bora, akina
mama wengi na vichanga tunaowapoteza kwa sasa wataokolewa. Kwa sasa wanawake
wanaojifungulia katika vituo vya afya bado ni wachache:
kwa mujibu
wa utafiti wa Demografia na Afya Tanzania (TDHS) 2010 ni mwanamke mmoja tu
katika kila wawili ndiye anayejifungulia katika kituo cha afya.
Yaani kigezo
cha hatua hii muhimu ambayo ingeweza kuchukuliwa na kupunguza vifo vya mama na
vichanga kwa kiasi kikubwa kimekuwa hivyo hivyo katika kipindi cha miaka 25
bila mabadiliko.
Hii ni tangu
ulipofanyika utafiti wa TDHS wa kwanza 1990 ambapo ni nusu tu ya wanawake
walikuwa wakijifungulia kwenye vituo vya afya.
Na japo kwa
usahihi kabisa, makala hii imeeleza kuhusu ongezeko la idadi ya vizazi hai
katika vituo vya afya, ieleweke kuwa pia ongezeko kubwa la idadi ya watu hapa
Tanzania linamaanisha kuwa mfumo wa afya nao haujaweza kufanya mabadiliko ya
kuendana na kiwango cha ongezeko la wanawake wanaojifungulia vituo vya afya
kati ya mwaka 1986 na 2010.
Ujumbe mkuu
hapa ni kuwa idadi kubwa ya akina mama na watoto wachanga wa Tanzania ambao
maisha yao yanapotea wakati wa ujauzito na kujifungua kila mwaka yangeweza, na
kwa hakika yanatakiwa kuokolewa.
Kila mtu,
kwa nafasi yake katika jamii ni lazima atambue fursa zilizopo, zinazoweza
kugeuza mwelekeo wa janga hili linalotokea kila siku.
MIMBA ZA UTOTONI, KIKWAZO KWA WASICHANA MBEYA, PWANI NA MARA
WAKATI
imebakia miaka miwili kuhakikisha malengo ya milenia yanatekelezwa, baadhi ya
watoto wa kike nchini Tanzania, wamekuwa wakifukuzwa shule kutokana na
ujauzito, huku wengine wakiacha wenyewe masomo pale tu wanapojigundua ni
wajawazito.
Maeneo
ambayo ymebainika kuwepo kwa hatari hiyo inayoendelea kwa watoto hao wa kike ni
wilayani Ileje, Kyela mkoani Mbeya, Musoma mkoani Mara na Bagamoyo mkoani
Pwani.
VIFAA TIBA, VYATOLEWA KWA MKOA WA MBEYA NA TANGA KWA AJILI YA MRADI WA AFYA YA MAMA NA MTOTO UNAOTEKELEZWA KWA USHIRIKIANO WA MFUKO WA TAIFA BIMA YA AFYA (NHIF) NA BENKI YA MAENDELEO YA WATU WA UJERUMANI-kfw
VIFAA HIVYO NA MAJINA YAKE LA,A
VINAVYOONEKANA. Vimekabidhiwa leo rasmi katika hafla fupi ya
makabidhiano iliyofanywa na Waziri wa Afya, Dr. Seif Rashid,
mkoani Mbeya.
Kulia ni Mratibu wa afya ya mama na mtoto, Prisca Butuyuyu, akibadilishana mawazo na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa mfuko wa bima ya Taifa ya bima ya Afya Hamis Mdee(kushoto), katika hafla fupi ya kukabidhi vifaa tiba kwa ajili ya mradi wa KFW.
Kulia ni Mratibu wa afya ya mama na mtoto, Prisca Butuyuyu, akibadilishana mawazo na Naibu Mkurugenzi Mkuu wa mfuko wa bima ya Taifa ya bima ya Afya Hamis Mdee(kushoto), katika hafla fupi ya kukabidhi vifaa tiba kwa ajili ya mradi wa KFW.
FAIDA ZA WAJAWAZITO KUJIFUNGULIA VITUO VYA AFYA HIZI HAPA
IKIWA mkoa
wa Mbeya una asilimia 57 ya wajawazito wanaojifungulia hospitali na vituo vya
afya, wito umetolewa kwao kujitokeza kwa wingi kuhudhuria Kliniki ili kupunguza
vifo vya mama na mtoto.
Wito huo
umetolewa mwishoni mwa wiki na Mhadhiri, kaimu mkuu wa taasisi ya tiba ya St.
Aggrey Jijini Mbeya, Dr. Karim Segumba.
Dr. Karim
alisema kuwa faida wanazozipata wajawazito wanapohudhuria Kliniki ni pamoja na mjamzito
kuchunguzwa afya yake kwa undani, ikiwemo umri wa mimba, kimo cha mimba,
historia ya uzazi wa awali, uwingi wa damu, mkojo kwa protini na kutoa wasiwasi
wa kifafa cha mimba.
‘’Mwanamke
anachunguzwa shinikizo la damu, mlalo wa mtoto, mapigo ya moyo ya mtoto,
ikibidi ultrasound kuangalia kama mtoto yupo hai, au ni mlemavu, ukubwa wa
mtoto, kondo la nyuma la mama, kukomaa kwa mtoto, nyonga za mama kama
zinaruhusu kujifungua kwa njia ya kawaida au upasuaji na anaelezwa tarehe ya
makisio ya kujifungua’’ alisema Dr. Karim.
Mbali na
uchunguzi huo, alisema kuwa mjamzito anayehudhuria kliniki anapimwa pia VVU na
anapoonekana kuwa ana maambukizi anapewa mbinu za kumkinga mtoto aliye tumboni.
Alipoulizwa madhara
yanayoweza kuwapata wajawazito ambao hawaendi kliniki na hawajifungulii
hospitali na vituo vya afya, alisema ni pamoja na mjamzito kutoelewa maendeleo
ya mimba yake na hatari ambazo zingeweza kugundulika na kutatuliwa na wataalam
ili kuzuia kifo chake na mtoto.
‘’Hivyo ili
kupunguza vifo vya mama na mtoto ni muhimu wajawazito wakahudhuria kliniki na
kujifungulia katika vituo vya tiba na kizuri zaidi huduma zote hizo kwa mama
mjamzito na mtoto chini ya miaka mitano hutolewa bure kote nchini’’ alisema
mhadhili huyo.
Mratibu wa
huduma ya mama na mtoto katika hospitali ya mkoa wa Mbeya Prisca Butuyuyu,
alisema kwa sasa mkoa wa Mbeya, wajawazito wengi wanahudhuria kliniki lakini
wengi wao wanajifunguli nyumbani.
Aliitaja wilaya
ya Ileje kuwa ndiyo wilaya inayoongoza kwa wajawazito kujifungulia nyumbani,
ambapo Jiji la Mbeya linaongoza kwa wajawazito wengi kujifungulia katika vituo
vya tiba.
‘’Zaidi ya
asilimia 40 wajawazito wanajifungulia nyumbani lakini baadhi wanajifungulia kwa
wakunga wa jadi na njiani ingawa hatuna takwimu sahihi zaidi’’ alisema
Butuyuyu.
Alisema Jiji
la Mbeya wajawazito wanajifungulia hospitali hasa hospitali ya wazazi Meta kwa
asilimia 109, Kyela 67, Chunya 58, Rungwe 55, Mbozi 45, Mbeya Vijijini asilimia
38 na wilaya ya Ileje asilimia 33.
WAJAWAZITO TANZANIA WAJIFUNGULIA MALAWI
TUJIKUMBUSHE MAKALA HII NA KUTAFAKARI
*Unafuu na kutotozwa fedha wala vifaa, kivutio tosha.
Na
Gordon Kalulunga.
SERA ya Afya ya mwaka 2007 haifahamiki wilayani
Ileje katika mkoa wa Mbeya. Ni katika sera hii ambamo inatamkwa kwamba
wajawazito nchini watapewa huduma za afya bure.
Kama sera inafahamika, basi haitekelezwi. Baadhi
ya wajawazito katika wilaya ya Ileje wanaacha zahanati, vituo vya afya na
hospitali wilayani mwao na kuvuka mpaka hadi nchini Malawi kufuata kinachoitwa
“huduma bora.”
Kwa mfano, wajawazito kutoka kata za Bupigu,
Itumba na Isongole wanafahamika kwa kwenda nchini Malawi kwa wingi ili waweze
kujifungulia huko na kupata huduma nyingine za afya.
Lakini kutoka Isongole hadi hospitali maarufu ya
Chitipa nchini Malawi ni umbali wa kilometa 45; wakati umbali wa kwenda
hospitali ya serikali ya Ileje ni kilomita tatu tu.
Mwanamke mkazi wa kijiji cha Ikumbilo, kata ya
Chitete wilayani Ileje, aliyejitambulisha kuwa anaishi na virusi vya ukimwi (VVU)
anasema aliwahi kujifungulia hospitali ya Chitipa na mpaka sasa anapata
matibabu yake huko.
Kuna nini katika hospitali ya Chitipa nchini
Malawi hadi wajawazito wakimbilie huko? Jibu analo Neema Mbughi mkazi wa kijiji
na kata ya Bupigu.
“Pale hospitali ya Chitipa hubebi chochote wakati
unakwenda kujifungua. Hatuendi na madishi, karatasi za nailoni (ambako mjamzito
huhala wakati wa kujifungua) wala glovu. Kila kitu ni bure, hata chakula
ambacho kimepikwa kama kimetoka nyumbani,” anaeleza Neema.
Friday 30 May 2014
DALILI 13 ZA MWANAMKE MJAMZITO
by Gordon
Kalulunga
TANGU niwe
mmoja wa waandishi wa habari 5 waliobahatika kufauru usaili kati ya waandishi
72 Tanzania na kujifunza na kubobea kuandika habari za afya ya uzazi nchini
Tanzania tangu mwaka 2012 nimejionea, nimesikia, nimegusa, nimenusa wakati
mwingine kuyaishi maisha na wanawake wajawazito na hata ambao bado hawajawa
wajawazito.
Nieleze wazi
kuwa mafunzo hayo niliyapata kupitia program ya Fellowship inayoratibiwa na
mfuko wa vyombo vya habari Tanzania maarufu kama Tanzania Media Fund (TMF) na
kufundishwa na madaktari bingwa wa masuala ya afya ya uzazi.
Moja ya
mambo ambayo nilijifunza kutoka kwa wataalamu hasa madaktari nikiwa field,
kusoma mitandao na baadhi ya wanawake waliosema wazi wazi kuhusu dalili za
ujauzito na kati ya nyingi nilizoelezwa kati yake 13 nimeona nikushirikishe
katika makala hii ya uchambuzi.
Mwanamke
anapopata ujauzito kwa kawaida huwa anaanza kuona dalili ambazo si za kawaida.
Na ni wakati huo ambao ni muafaka kwake kuanza kuuchunguza mwili wake.
Inaonesha
kuwa homoni zinazosambaa mwilini mara tu unapopata ujauzito husababisha
mabadiliko kadhaa katika mwili wake ambayo yanaweza kugundulika kabla hata ya
uchunguzi halisi wa kujua kama mjauzito au la.
1. Maumivu
kwenye matiti.
Hii ni
dalili ya kawaida ya ujauzito ambapo nguvu za homoni mwilini huongezeka wakati
yai linavyopata “rutuba”, jambo ambalo huongeza wingi wa damu na kuyafanya
matiti ya mwanamke kuvimba na kuwa makubwa isivyo kawaida.
2. Maumivu
mwilini
Baadhi ya
wznawake wanajisikia maumivu kama vile wanataka kuingia katika siku zao. Kwa
kawaida hali hii hutokea wakati yai likiwa linasafiri kwenda katika chumba cha
mimba. Hivyo, hali hiyo husababisha sehemu hiyo itanuke taratibu na kusababisha
maumivu hayo.
3. Kutokwa
damu bila kutegemea
Wanawake
wengi hufikiria kutokwa na damu kidogo ni dalili ya kuwa katika siku zao.
Lakini, katika hali halisi, kutokwa damu kusikotegemewa, huwakumba asilimia 25
ya wanawake wakati wa kurutubika kwa yai na iwapo utaona hedhi inakuwa fupi au
inafanyika katika hali ambayo si ya kawaida, mwanamke anashauriwa kwenda
kufanya kipimo cha ujauzito au kujipima mwenyewe na kifaa cha kupimia
ujauzito..
4. Kuchoka
Mwanamke
anapojisikia kuchoka na kukosa raha, au kutaka hata kulala wakati akiwa kazini,
wakati huo mwili wake unakuwa unajirekebisha kuingia katika kipindi kipya cha
mabadiliko.
Inaelezwa
kuwa katika kipindi cha mwanzo cha ujauzito ni muda ambao mtoto tumboni huanza
kutumia sehemu ya nguvu za mwanamke na hivyo kumletea uchovu na usingizi.
5. Chuchu
kuwa nyeusi
Chuchu
huanza kubadilika rangi yake kutokana na chembechembe za uhai (seli) kuanza
kufanya kazi kwa nguvu zaidi hata hivyo wanawake wenye ngozi nyeusi hawawezi
kuiona dalili hii mapema hadi muda wa kama wiki kumi zipite.
Hali hii
huwapata asilimia 85 ya wanawake wanapopatwa na ujauzito, ambapo nyakati za
asubuhi ndipo hasa hujionyesha.
7. Mwili
kuvimba
Kuna wakati
kupungua kwa nguvu za uyeyushaji chakula kunaweza kumsababishia mwanamke kuona
tumbo limevimba na nguo zikawa zinambana kutokana na chakula kujaa katika
utumbo. Lakini hali hiyo ikiendelea na ukaona siku zako haziji, basi ni vyema
ukatambua kwamba tayari una ujauzito na kinachokupasa ni kwenda kuhakikisha.
8. Kwenda
haja ndogo mara kwa mara
Mwanamke
kwenda haja ndogo kila mara ni dalili kwamba kibofu kimeanza kufanya kazi ya
ziada, ambapo huwa kinafanya kazi ya kuondoa maji kwa uthabiti zaidi wakati wa
ujauzito.
Hali hii pia
hujitokeza mwishoni mwa ujauzito, ambapo kibofu kitakapokuwa kinarudia hali
yake ya kawaida baada ya kufanya kazi kwa muda mrefu.
Kutokana na
mwili kuwa na “mzigo” wa ujauzito na hivyo kuchoka, hali hiyo humfanya mwanamke
kutamani vitu mbalimbali ili kukidhi mabadiliko yaliyojitokeza katika mwili
wake. Hii ni pamoja na kutaka vyakula fulani au kufanya mambo ambayo hapo nyuma
alikuwa hayapendi.
10. Kuumwa
kichwa
Kuongezeka
kwa damu kunaweza kusababisha kichwa kuuma japokuwa si sana, hususani katika
wiki za mwanzo za ujauzito. Hata hivyo, hali hii hukoma mwili unapojirekebisha
na mzunguko wa homoni unaotokana na ujauzito.
11. Kufunga
choo.
Homoni
ambazo husababisha mwili kuvimba pia husababisha kufunga choo kutokana na mfumo
wa kuyeyusha chakula kutofanya kazi vyema. Hata hivyo hali hii inaweza
kujitokeza zaidi wakati ujauzito unapoendelea kukua.
12. Kuwa na
hasira
‘’Kutokana
na kuongezeka kwa homoni za utendaji kazi mwilini, hali hiyo itakusababishia
uchovu, na kukufanya kuwa na hasira,”anasema Melissa Goist, Profesa na Mtalaama
wa Masuala ya Uzazi wa Chuo Kikuu cha Ohio, Marekani.
Kipimo cha
joto la mdomo ni muhimu katika kutambua hali ya ujauzito. Kwa kawaida joto
huongezeka kwa nyuzi moja au zaidi wakati yai likiwa linatunga mimba. Hali hiyo
ikiendelea kwa zaidi ya wiki mbili, itakuwa inaonyesha dhahiri kwamba kuna
“mtoto anakuja”.
0754 440749
MAMBO MUHIMU AMBAYO UNATAKIWA UYAFANYE KABLA YA KUOA AU KUOLEWA
Dr, Pastor,
Gordon Kalulunga.
MOJA ya mambo ambayo yanakosekana katika nyumba za ibada ni mafundisho ya mahusiano.
Watu wengi
hawajui kuwa mtu aliyeolewa na hajaolewa au kuoa, ana haki ya kupata elimu ya
ndoa.
Unaweza
kujiuliza kuwa kwanini ndoa nyingi zina shida? Jawabu ni kwamba wengi wanajua
ndoa baada ya kuingia kwenye ndoa, hawajawahi kupata elimu ya mahusiano.
Ni sawa na
kumfundisha dereva kuendesha gari.
Wengi wamekosa
elimu ya mahusiano au kuoa au kuolewa, vijana na mahusiano, bali wengi wana
elimu za upako wa mafanikio na toa ndugu toa ndugu ndiyo masomo tuliyoyazoea.
Mfumo wa
elimu tuliyonayo nao ni tatizo. Kwa mfano kwenye Biblia hakuna neno linalosema
rafiki au mchumba.
Huwezi
kukuta kitu kinachoitwa, urafiki, uchumba baadaye ndoa.
Ngoja
nikuambie, Mathayo Mtakatifu sura ya 1;1-23. Mariamu alipoposwa….. haisemi
alichumbiwa! Lakini katika utamaduni wa kimagharibi leo hii watu wanasema kuwa
mchumba wa Yusufu.
Mchumba huwa
anapimwa, ndiyo maana watu wanakuwa na wachumba wengi kweli na hatimaye uchumba
unavunjika kwasababu hakuna mtu anayeenea kwenye utimilifu.
Kuna fix za
kifikra ambazo zina ugonjwa wa kufisha, kesho unaweza kulia ukiendekeza
kumtafuta mchumba badala ya kumtafuta mume au mke.
Akina dada
wengi wanaomba na kusugua magoti wakiomba wapate wachumba.
Maandiko
yanasema kuwa, ‘’Mjibu mpumbavu kutokana na upumbavu wake’’
Mtu ana
wachumba kadhaa, kisha anaanza kumuomba Mungu ampe mume au mke huku akiwa na vinyago
vyake. Majibu yatakuja kama anavyowaza.
Yaani tayari wana fikra, vinyago na maamuzi yao kati ya wale wachumba waliopo moyoni na kichwani.
Yaani tayari wana fikra, vinyago na maamuzi yao kati ya wale wachumba waliopo moyoni na kichwani.
Mungu
atamjibu mtu kutokana na elimu aliyonayo ya urafiki, uchumba kisha ndoa.
Walio kwenye ndoa wengi wanajuta kwasababu
wameoa au kuolewa na rafiki….
Ukikaa na
mtu utasikia anakuambia, mtumishi nimeumia, tunakuabudu Bwana, utafikiri upako
umetembea, kumbe watu wana kesi zao na nafsi zao zimepigwa.
Mimi kama
mwalimu ambaye sawa na Daktari, nikianza kufuatilia ninajua.
Ukimuuliza
vipi ina maana una chimichimi ya roho mtakatifu ndiyo maana kila tunapoanza
kuabudu analia?
Ukidadisi
mtu anakumbia kuwa, nilikuwa na mchumba akaniambia utanioa, akamwambia na
rafiki yangu na mwingine…..
Nafsi za
watu wa Mungu nyingi zimeumizwa na kuna kesi nyingi za kuachwa kuliko kesi za
uhalifu mwingine.
Ukiomba
mchumba, wanaweza kuja wengi kisha unapoanza kuburuzana nao unachoka kisha
unatumbukia popote…..
Jambo hili
la ndoa na uchumba ni gumu kwasababu vijana wengi ni wavivu kujifunza maandiko
ya Mungu bali wanataka watafuniwe kila kitu na kulishwa.
Mungu ni
roho, alimuumba mtu kwa mfano wake, akasema nendeni duniani mkazae na
kuongezeka. Maandiko yanaposema Mtu, ina maanisha mfano wa roho.
Kwenye
ulimwengu wa roho, Mungu aliumba mtu mke na mtu mume na ndiyo maana amekataza
kuzini.
Maana yake
ni kwamba kila mmoja ana mke wake na ana mume wake kwasababu kila mmoja
aliumbwa na wake.
Ukiishika
elimu hiyo, hautalia kwasababu eti hujapata mume au mke. Mbinguni kuna roho
nyingi zinazataka kuja duniani, hivyo tuliopo tumepata neema ya kutangulia
kuzaliwa.
Unapomuona
mwanaume anapita, ujue kuwa huyo ni mume wa mtu na mwanake anayepita ni mke wa
mtu.
Tatizo watu
wanaomba kwa Mungu wapate mke au mume huku wakilia!
Inashangaza mtu unaenda kudai deni lako huku akilia. Maana yake hajui haki yake, yaani imani zetu hazijawa sawa.
Inashangaza mtu unaenda kudai deni lako huku akilia. Maana yake hajui haki yake, yaani imani zetu hazijawa sawa.
Kama ndani
yako una usongo wa kuoa au kuolewa, fanya hivi. Kwa imani nenda kamnunulie na
suti iweke ndani maana kwa imani yupo.
Acha kushika yeyote mwisho utashika hata majoka.
Acha kushika yeyote mwisho utashika hata majoka.
Mungu
hupendezwa na mtu mwenye imani na anamletea. Acha kulia.
Wanaume
ngoja niwaambie. Mungu alipokuwa akiumba, alimtanguliza Brother men, kisha
akamlaza usingizi na kuchomoa ubavu akamtengeneza mwanamke. Maana yake ni
kwamba mwanamke wa kwako yupo, labda uwe towashi.
Wanawake
hampaswi kufifia ngozi kwamba hamtaolewa, maana usigeweza kuumbwa bila wa kwako
kuwepo na wala hajafa bali yupo, cha kufanya amini. Kanunue na suti kaweke
ndani, anza kufanya maandalizi…
Kuweni na imani
inayowekwa kwenye matendo, msiamni kuwa mtakosea.
Sehemu
nyingine huwa nawafundisha kuwa, ukishatambua kuwa wa kwako yupo, tulia au
subiri.
Kwa kuwa
hatuamini kuwa wa kwako yupo, hatutulii, na kwa kuwa tunaanza kaba ya majira na
wakati ndipo tunapoeekea kwenye kuumia na majuto ya uchumba na ndoa.
Wimbo
uiobora 3;5 ….msiyachochee mapenzi wala kuyaamsha……Mungu anasema hayo kwasababu
kabla ya Mungu kuyaamsha, wewe unawahi.
Mfano;
Sekondari mtu hasa wanawake, anapokuwa kidato cha pili tu au kabla ya hapo,
anaanza kuomba, Mungu nipe Mume….. hebu jiulize wewe ulianza lini kuzitikisa
mbingu za mapenzi…… jibu unalo.
Wanyakyusa
wanao usemi kwa mtu mzima anayefanya mambo ya hovyo, unasema…..amakambo,
akwesile ndili… yaani mtu huyo anasumbuliwa na bangi….alivuta lini?
Hapa
namaanisha kuwa unaweza kukimbilia na ukapata mume maana hakuna mtu anayekuwa
anazijua tabia za wenzake, kisha utaanza kusema kuwa aaaaa…kumbe hakuwa
mwenyewe..
Ibrahimu
haraka zake zinasumbua kule Israel mpaka leo.
Niwaambie ukweli kuwa haraka zina hasara zake sawa na utunzaji wa mtoto njiti ni kazi kubwa.
Hivyo ukiharakisha unaweza kupata mume au mke njiti…
Niwaambie ukweli kuwa haraka zina hasara zake sawa na utunzaji wa mtoto njiti ni kazi kubwa.
Hivyo ukiharakisha unaweza kupata mume au mke njiti…
Sijui kama
ninaeleweka katika somo hili. Haraka zinaendana na akina dada kuongea
harakaharaka, wanaume wengi hawapendi mwanamke wa namna hiyo.
Yesu aliwahi
kujaribiwa na kahaba, mafarisayo miili yao ikawa nyang’anyang’a huku yule
kahaba akitoa machozi na kufuta miguu ya Yesu kwa nywele zake, hivi ungekuwa
wewe Brother men ungefanyaje hapo?
Usiwe na
haraka. Watoto wa kike ndo wana speed kuliko hata dunia inavyozunguka jua.
Hamnoni
alimpenda Tamali mpaka akaumwa…. Lakini baada ya kulala naye akamchukia na
kumwambia Tamali aondoke na akamchukia kwelikweli…..tafakari.
Hapa
kinachotendeka katika ulimwengu wa roho ni kependa umbo lakini my akionja hakuti
kile ambacho alikuwa anakifikiri.
Mfano mzuri
ni kwamba wanaume na wanawake wengi ambao wamedumu katika mapenzi hawaoani.
Mwanaume
akitembea na mwanamke na kutokukuta alichokitarajia, anasema hata kwa wenzake
kuwa ‘’demu mwenyewe mshamba na hana lolote’’ yote hiyo ni kuyachochea mapema
na kuvua.
Nitajuaje
kama ndiye?
Kimaandiko
unapomuomba Mungu, utawekewa rohoni kitu kinachoitwa mwongozo.
Utaona
unasukumwa na jambo la kuolewa kama kuku navyosumbuka kutafuta eneo la kutagia,
sawa na mtumishi wa Mungu anapotaka kufanya jambo la kiroho.
Jifunze
kumsikiliza Mungu, ondoa moyoni kufikiri kuwa huyo unayefikiri na kumweka
moyoni kama ni mwenyewe, huyo siyo.
Achana naye maana roho ya mauti ipo juu yako. Tubu.
Achana naye maana roho ya mauti ipo juu yako. Tubu.
MSIKILIZE
MUNGU ILI ASIKUJIBU SAWA SAWA NA VINYAGO ULIVYOWEKA MOYONI MWAKO NA KUJIINGIZA
POPOTE.
HEBU JIULIZE, MPAKA SASA UNA VINYAGO VINGAPI?
HEBU JIULIZE, MPAKA SASA UNA VINYAGO VINGAPI?
Hili ni somo
la sikio halisi, siku nyingine nitatoa mifano yangu halisi…..
Mungu awabariki na awasamehe wote
wenye toba.
Gordon Kalulunga
Information and Media
Consultant
P.O. Box 705,
Mbeya-Tanzania
Tel: 255 (0)754 440749
e-mail: kalulunga2006@gmail.com
WEB; www.kalulunga.blogspot.com
Subscribe to:
Posts (Atom)